Home About Articles Ask the Sheikh
Maswali na Majibu

Jibu la Swali: Hukumu ya Mikataba Miwili ya Duwayani na Nisfagi Maarufu Nchini Afghanistan

March 03, 2017
4044

Silsila ya Majibu ya Mwanachuoni Mtukufu Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, Ameer wa Hizb ut Tahrir kwa maswali ya wafuasi wa ukurasa wake wa Facebook "Fiqhi"

Jibu la Swali

Kwa Abdul Jamil Qame'

Swali:

Assalamu Alaikum...

Sheikh wetu mtukufu, tuna muamala nchini Afghanistan ambao hatujui usahihi wake na umeenea sana, na mfumo wake ni: Kwamba maskini anachukua ndama mwenye umri wa mwaka mmoja au miezi kumi anamfuga kwa mwaka mmoja au miwili, na ikiwa ni jike akapata mimba na kuzaa, basi maskini anachukua ndama wake na maziwa yake na kumkabidhi ng'ombe huyo kwa mmiliki wake, au wanamuuza kwa nusu kwa nusu kabla ya kuzaa. Na ikiwa ni dume, wanamuuza kwa nusu kwa nusu au wanambaki naye na kugawana manufaa yake nusu kwa nusu. Surah ya kwanza inaitwa Duwayani na surah ya pili inaitwa Nisfagi. Je, mkataba huu ni batili au ni sahihi?

Na Jazakumullah Khayra.

Jibu:

Walaikum Assalam Wa Rahmatullahi Wa Barakatuh,

Hakika miongoni mwa masharti ya ijarah (ajira) katika Uislamu ni kwamba ujira unapotajwa lazima uwe unajulikana (ma'lum) na usiwe usiojulikana (majhul). Imekuja katika kitabu cha Mfumo wa Kiuchumi, mlango wa "Ujira wa Kazi", ukurasa wa 91: (...na inashartiwa kuwa mali ya ujira iwe inajulikana kwa kuonekana na kwa sifa inayoziondoa kutojulikana, kwa sababu Mtume ﷺ alisema:

إِذَا اسْتَأْجَرَ أَحَدُكُمْ أَجِيراً فَلْيُعْلِمْهُ أَجْرَهُ

"Mmoja wenu anapomajiri mwajiriwa, basi amjulishe ujira wake."

Na malipo ya ujira inaruhusiwa kuwa ni pesa, na inaruhusiwa kuwa si pesa, na inaruhusiwa kuwa ni mali, na inaruhusiwa kuwa ni manufaa, na kila kilichoruhusiwa kuwa ni thamani (katika biashara) kinaruhusiwa kuwa ni malipo (katika ajira), kwa sharti kwamba iwe inajulikana. Ama ikiwa haijulikani basi haisihi. Hivyo, ikiwa atamajiri mvunaji kwa sehemu isiyojulikana ya mazao haisihi kwa sababu ya kutojulikana, tofauti na ikiwa atamajiri kwa pishi moja au mudi mmoja, hapo itasihi. Na inajuzu kumajiri mwajiriwa kwa chakula chake na mavazi yake, au kumwekea ujira pamoja na chakula chake na mavazi yake. Kwa sababu hilo linajuzu kwa mnyonyeshaji, Amesema Ta’ala:

وَعَلَى الْمَوْلُودِ لَهُ رِزْقُهُنَّ وَكِسْوَتُهُنَّ بِالْمَعْرُوفِ

"Na ni juu ya baba chakula chao na nguo zao kwa mujibu wa ada." (QS Al-Baqarah [2]: 233)

Hivyo amewawekea matumizi (nafaka) na mavazi juu ya unyonyeshaji. Na ikiwa inajuzu kwa mnyonyeshaji, basi inajuzu kwa mwengine, kwa sababu yote hayo ni ijarah, nayo ni suala miongoni mwa masuala ya ijarah...)

Matokeo yake ni kwamba ni lazima ujira unapotajwa uwe unajulikana elimu inayokanusha kutojulikana, ili iweze kutekelezwa bila ya mzozo. Kwa sababu asili katika mikataba yote ni kuondoa mizozo kati ya watu. Na kwa ajili hiyo inashartiwa ujira uwe unajulikana kwa kauli yake ﷺ: «Mmoja wenu anapomajiri mwajiriwa, basi amjulishe ujira wake» amepokea Ad-Daraqutni kutoka kwa Ibn Mas’ud, na kutokana na aliyopokea Ahmad kutoka kwa Abu Said kwamba Mtume ﷺ:

نَهَى عَنِ اسْتِئْجَارِ الأَجِيرِ حَتَّى يُتَبَيَّنَ لَهُ أَجْرُهُ

"Alikataza kuajiri mwajiriwa mpaka ubainishwe kwake ujira wake."

Isipokuwa kwamba ikiwa ujira haukujulikana, ijarah hufungika na kusihi, na hurejelewa wakati wa hitilafu katika kiasi chake kwenye ujira wa mfano... Na mada hii kwa ukamilifu imetajwa katika Mfumo wa Kiuchumi katika mlango wa Ijarah, na inaweza kufuatiliwa huko.

Na kwa kuzingatia hilo, swali lako kama nilivyolielewa ni kama ifuatavyo:

Maskini anayechukua ndama mwenye umri wa mwaka mmoja au miezi kumi, kisha anamfuga na kumtunza kwa mwaka mmoja au miwili, na ujira wake unakuwa:

** Ikiwa ndama aliyechukuliwa ni jike na akamtunza mpaka akawa ng’ombe, basi katika hali hii:

a- Ikiwa atazaa katika kipindi cha ufugaji, basi ujira wa maskini ni yule ndama aliyezaliwa, na maziwa yake, kisha anamkabidhi ng’ombe huyo kwa mmiliki wake...

b- Au achukue nusu ya thamani ya ng’ombe huyo wakati wa kuuzwa kwake kabla ya kuzaa kama ujira wake, badala ya ufugaji wa kipindi hicho.

** Ikiwa ndama aliyechukuliwa ili amfuge na kumtunza ni dume, basi ujira wake unakuwa baada ya kumfuga kwa mwaka mmoja au miwili:

c- Wanamuuza na thamani yake ni nusu kwa nusu baina yao.

d- Au wanambaki naye na kugawana manufaa yake baina yao nusu kwa nusu.

Ikiwa niliyoyaelewa kama ilivyo hapo juu ni sahihi, basi hukumu ya kisheria katika hali hii inategemea kuwa kwa ujira unajulikana, na si usiojulikana, na kwamba muda wa utunzaji na ufugaji kadhalika uwe umewekwa wazi na unajulikana, na jibu ni kama ifuatavyo:

  • Kipengele "a", haijuzu mkataba ndani yake, kwa sababu ujira ni kile atakachobeba jike huyo na hicho hakijulikani...

  • Kipengele "b" ujira unajulikana kwa sababu ni nusu ya thamani ya ng’ombe wakati wa kuuzwa katika muda uliokubaliwa, hivyo inajuzu.

  • Kipengele "c" ujira unakuwa nusu ya thamani ya ndama wakati wa kuuzwa katika muda uliokubaliwa na hili linajuzu.

  • Kipengele "d" lazima yaainishwe manufaa yanayogawanywa nusu kwa nusu ili yawe yanajulikana kwa wazi ili ijuzu, na ikiwa hayajulikani basi haijuzu.

Ndugu yenu Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah

03 Jumada al-Thani 1438 H Sawa na 02/03/2017 M

Link ya jibu kutoka kwa ukurasa wa Ameer kwenye Facebook

Link ya jibu kutoka kwa ukurasa wa Ameer kwenye Google Plus

Link ya jibu kutoka kwa ukurasa wa Ameer kwenye Twitter

Link ya jibu kutoka kwa ukurasa wa Ameer Web

Share Article

Share this article with your network