Home About Articles Ask the Sheikh
Maswali na Majibu

Jibu la Swali: Kuhusu Matumizi ya Makhalifa Waongofu ya Bendera ya al-Uqab na al-Liwa

May 26, 2013
6956

(Mfululizo wa majibu ya mwanachuoni Ata bin Khalil Abu Al-Rashtah, Ameer wa Hizb ut Tahrir, kwa maswali ya wafuasi wa ukurasa wake wa Facebook)

Kwa al-Wathiq bi-Nasrillah

Swali:

Assalamu Alaikum wa Rahmatullahi wa Barakatuh

Je, imepokelewa kwamba Makhalifa Waongofu walinyanyua bendera ya al-Uqab na al-Liwa? Na je, hili limeelezwa katika mapokezi (athar)? Allah awabarikini.

Jibu:

Wa Alaikum Salam wa Rahmatullahi wa Barakatuh,

Ndiyo ndugu yangu, Makhalifa Waongofu walikuwa wakitumia bendera ya al-Uqab na al-Liwa. Ama dalili za hilo ni kile kilichopokelewa kutoka kwa Mtume wa Allah (saw) kwamba bendera yake (rayah) ilikuwa ni al-Uqab na bendera yake (liwa) ilikuwa nyeupe, na miongoni mwa dalili hizi ni:

1- Al-Nasai ametoa katika Sunan al-Kubra, na al-Tirmidhi kutoka kwa Jabir, kwamba Mtume (saw):

دَخَلَ مَكَّةَ وَلِوَاؤُهُ أَبْيَضُ

"Aliingia Makka na bendera yake (liwa) ikiwa nyeupe." (Sunan al-Nasai al-Kubra na al-Tirmidhi).

Pia Ibn Abi Shaybah ametoa katika Musannaf yake kutoka kwa Amrah, amesema:

كَانَ لِوَاءُ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَبْيَضَ

"Bendera ya Mtume wa Allah (saw) (liwa) ilikuwa nyeupe." (Musannaf Ibn Abi Shaybah).

2- Ahmad, Abu Dawood, na al-Nasai katika Sunan al-Kubra wametoa kutoka kwa Yunus bin Ubayd, mtumwa wa Muhammad bin al-Qasim, amesema: Muhammad bin al-Qasim alinituma kwa al-Bara bin Azib kumuuliza kuhusu bendera (rayah) ya Mtume wa Allah (saw) ilikuwa vipi? Akasema:

كَانَتْ سَوْدَاءَ مُرَبَّعَةً مِنْ نَمِرَةٍ

"Ilikuwa nyeusi, ya mraba, iliyotengenezwa kwa kitambaa cha sufu (namirah)." (Musannaf Ahmad na Sunan Abu Dawood).

3- Al-Tirmidhi na Ibn Majah wametoa kutoka kwa Ibn Abbas amesema:

كَانَتْ رَايَةُ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ سَوْدَاءَ، وَلِوَاؤُهُ أَبْيَضَ

"Bendera (rayah) ya Mtume wa Allah (saw) ilikuwa nyeusi, na bendera yake (liwa) ilikuwa nyeupe." (Sunan al-Tirmidhi na Sunan Ibn Majah).

4- Ibn Abi Shaybah ametoa katika Musannaf yake: kutoka kwa al-Hasan, amesema:

كَانَتْ رَايَةُ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ سَوْدَاءَ تُسَمَّى الْعُقَابَ

"Bendera (rayah) ya Mtume (saw) ilikuwa nyeusi ikiitwa al-Uqab." (Musannaf Ibn Abi Shaybah).

Inatosha kuwa dalili kwamba Makhalifa Waongofu walimfuata Mtume wa Allah (saw) katika Rayah na Liwa, kwani wao hawakuwa wakiacha jambo lolote alilolitangaza Mtume (saw) miongoni mwao isipokuwa walilitekeleza. Na hakuna haja ya utafiti zaidi kuhusu Rayah na Liwa katika enzi ya Makhalifa Waongofu kwa sababu ya mambo mawili:

Kwanza: Kwamba hukmu ya kisheria inachukuliwa kutoka kwa Mtume (saw).

Pili: Kwamba Makhalifa Waongofu hawaachi jambo lililoshuhudiwa akilifanya Mtume (saw) kama vile Rayah na Liwa.

Ndugu yenu Ata bin Khalil Abu Al-Rashtah

Kiungo cha jibu kutoka kwenye ukurasa wa Ameer wa Facebook

Kiungo cha jibu kutoka kwenye tovuti ya Ameer

Kiungo cha jibu kutoka kwenye ukurasa wa Ameer wa Google Plus

Share Article

Share this article with your network