Mfululizo wa majibu ya mwanachuoni mtukufu Ata bin Khalil Abu Al-Rashtah, Amir wa Hizb ut-Tahrir, kwa maswali ya wafuasi wa ukurasa wake wa Facebook "Fiqhi"
Jibu la Swali
Kwa Ashraf Bader
Swali:
Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh Amir wetu mtukufu, nakuomba Allah Aliyekuwa Juu na Muweza akupe afya na uzima, na nakuomba Allah akusaidie na kukuimarisha. Ningependa kuwasilisha mada ambayo nakuomba Allah aniwafikishe kwayo, na ingekuwa vyema kama mgeitazama na kuamua kuihusu.
Imepokewa katika kitabu cha Ash-Shakhsiyyah Al-Islamiyyah Juzuu ya Kwanza katika mlango wa "Haja ya Umma leo kwa Wafasiri" (haja al-ummah al-yawm ila mufassirin) tulipozungumzia kuhusu Waarabu kutosheka na baadhi ya maneno badala ya visawe vyake au yanayokaribiana nayo madamu maana iliyokusudiwa inanyooka. Na katika mada ya Qira'at, tulitoa mfano katika ukurasa wa 309 na ninahisi kuwa tumekosea kidogo hapo, nao ni kauli Yake Aliyetukuka "لنبوئنهم من الجنة غرفا" tulipoiunganisha na Qira'a ya Abu Ja'far kutoka katika riwaya zake mbili "لنبوينهم من الجنة غرفا" na hii ni kwa sababu mbili:
Kwanza: Ni kweli kwamba Abu Ja'far anasoma kwa kubadilisha hamza kuwa ya, lakini anasoma kwa kuunganisha mim ya wingi (silat mim al-jam') bila pingamizi "لنُبَوِّیَنَّهُمُ من" na hivyo basi, kuingiza (idgham) kwa mim ya "نبوینهم" kwenye mim ya "من" kunaondoka kama ilivyoonyeshwa katika kitabu ukurasa wa 309, na kusoma kwa kubadilisha (ibdal) pamoja na idgham ya mim haijapokewa katika Qira'at yoyote mutawatir. Jambo jingine ni kwamba hukumu ya ibdal haathiri maana ya neno na ni katika hukumu za misingi (usul). Na madamu mada inahusu Waarabu kutosheka na maneno badala ya visawe vyake au yanayokaribiana nayo, basi huu haufai kuwa mfano, kwa sababu maana ya "بوأ" na "بوا" haitofautiani kwani neno ni lile lile lakini ni kwa hukumu ya ibdal.
Pili: Mfano ungeswihi ikiwa tungebadilisha Qira'a ya Hamza au Al-Kisa'i au Khalaf al-Asher badala ya Qira'a ya Abu Ja'far. Hii ni kwa sababu wao wanaisoma "لَنُثْوِیَنَّهُمْ من الجنة غرفا". Na neno "الثواء" linatofautiana na "التببوئة" kulingana na asili yake, na hivi ndivyo muktadha unavyohitaji. Allah ndiye Mjuzi zaidi. Ewe Allah ikiwa nimepatia basi ni kutoka Kwako na ikiwa nimekosea basi ni kutoka kwangu mwenyewe. Namuomba Allah atujalie miongoni mwa wale wanaochangia katika kuhifadhi utamaduni (tsaqafah) huu ukiwa safi. Allah akulipe kheri na akusaidie na kukuimarisha.
Jibu:
Wa Alaykum Salam Warahmatullahi Wabarakatuh, na Allah akubariki kwa dua yako njema kwetu...
Hakika swali lako, au tuseme maoni yako, ni kuhusu sehemu ifuatayo katika kitabu cha Ash-Shakhsiyyah Al-Islamiyyah Juzuu ya Kwanza:
[... Ama kwa upande wa mabadiliko katika maneno yakiwa ndani ya miundo yake, au mabadiliko katika miundo yenyewe, hakika Qur'ani imefuata desturi ya Waarabu ambao Qur'ani iliteremka kwa lugha yao. Na pamoja na muujiza wa Qur'ani kwa Waarabu, hakuna ukengeufu uliofanyika kutoka kwenye desturi yao iliyozoeleka katika mabadiliko ya usemi, na uhalisia wake katika upande huu ni ule ule wa desturi ya Waarabu katika hilo...
Na hilo limetokea katika Qur'ani kwa kutosheka na baadhi ya maneno badala ya visawe vyake au yanayokaribiana nayo kama vile Qira'at katika Qur'ani:
مَٰلِكِ يَوۡمِ ٱلدِّينِ "Mfalme wa Siku ya Malipo." (QS. Al-Fatihah [1]: 4)
مَلِكِ يَوۡمِ ٱلدِّينِ "Mfalme wa Siku ya Malipo." (QS. Al-Fatihah [1]: 4)
وَمَا يَخۡدَعُونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ "Wala hawadanganyi ila nafsi zao." (QS. Al-Baqarah [2]: 9)
وَمَا يُخۡادِعُونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ "Wala hawadanganyi ila nafsi zao." (QS. Al-Baqarah [2]: 9)
لَنُبَوِّئَنَّهُم مِّنَ ٱلۡجَنَّةِ غُرَفاً "Hakika tutawaweka katika maghorofa ya Peponi." (QS. Al-Ankabut [29]: 58)
لَنُبَوِّيَنَّهُم مِّنَ ٱلۡجَنَّةِ غُرَفاً "Hakika tutawaweka katika maghorofa ya Peponi." (QS. Al-Ankabut [29]: 58)
na aya nyinginezo kulingana na Qira'at] Mwisho.
Nawe unaona kuwa katika kitabu cha Ash-Shakhsiyyah Al-Islamiyyah Juzuu ya Kwanza kuna makosa katika maeneo mawili:
Kwanza: Kufanya mim ya (لنبوينهم) katika kitabu kuwa na sukun jambo ambalo linapelekea kuingizwa kwake (idgham) katika mim inayofuata katika herufi (من), na hivi ndivyo mim ilivyoonekana katika herufi (مّن) ikiwa na shadda katika kitabu na hivyo kuashiria idgham, na hili si sahihi kulingana na maoni yako kwa sababu (لنبوينهم) ambayo ni ya Abu Ja'far inasomwa kwa silat mim al-jam' hivyo hakuna idgham ya mim ndani yake.
Pili: Kwamba kutoa mfano kwa Qira'a ya (لنبوينهم) haufai kwa sababu neno (لنبوئنهم) ni sawa na neno (لنبوينهم) katika maana na kila kilichotokea ni kubadilishwa kwa hamza na kuwekwa ya mahali pake, na hili haliingiliani kulingana na maoni yako na jambo lililokusudiwa kutolewa mfano.
Na jibu la hilo ni kama ifuatavyo:
1- Kuhusu maoni yako ya kwanza, yaani kutokea kwa shadda kwenye mim katika herufi (مّن), jambo ambalo linamaanisha idgham ya mim ya (لنبوينهم) kwenye mim ya (من), na hii ni kinyume na Qira'a iliyotajwa ya Abu Ja'far kwa sababu yeye anasoma kwa kuunganisha mim ya wingi yaani anasoma (لنُبَوِّیَنَّهُمُ مِن), hivyo haingizi mim ya kwanza kwenye ya pili... Maoni haya ni sahihi, kwani imepokewa kuhusu Qira'a ya Abu Ja'far:
An-Nushur fi al-Qira'at al-Ashr (1/273) وَاخْتَلَفُوا فِي صِلَةِ مِيمِ الْجَمْعِ بِوَاوٍ وَإِسْكَانِهَا، وَإِذَا وَقَعَتْ قَبْلَ مُحَرَّكٍ "Na wakatofautiana katika kuunganisha mim ya wingi kwa waw na kuisukumia, na inapoanguka kabla ya herufi yenye haraka..." kama vile "أَنْعَمْتَ عَلَيْهِمْ غَيْرِ الْمَغْضُوبِ عَلَيْهِمْ", "وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنْفِقُونَ", "عَلَيْهِمْ أَأَنْذَرْتَهُمْ أَمْ لَمْ تُنْذِرْهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ", "عَلَى قُلُوبِهِمْ وَعَلَى سَمْعِهِمْ وَعَلَى أَبْصَارِهِمْ غِشَاوَةٌ وَلَهُمْ عَذَابٌ" فَضَمَّ الْمِيمَ مِنْ جَمِيعِ ذَلِكَ، وَوَصَلَهَا بِوَاوٍ فِي اللَّفْظِ وَصْلاً ابْنُ كَثِيرٍ وَأَبُو جَعْفَرٍ "basi akaidhumisha mim kutoka katika yote hayo, na akaiunganisha kwa waw katika tamko kwa muunganisho Ibn Kathir na Abu Ja'far."
Faridat ad-Dahr fi Ta'sil wa Jam' al-Qira'at (4/73) Qira'a: (2)... أبو جعفر بقراءة لنبوينهم بإبدال الهمزة ياء مفتوحة وصلة الميم. "...Abu Ja'far kwa qira'a ya lanubawwiyannahum kwa kubadilisha hamza kuwa ya yenye fatha na kuunganisha mim."
Kwa hiyo, kilichopo katika kitabu ni kosa la uchapishaji, na hakikuwepo katika matoleo ya awali ya kitabu cha Ash-Shakhsiyyah Al-Islamiyyah Juzuu ya Kwanza. Kwa mfano, toleo la tatu halikuwa na haraka kwenye herufi na matini ya aya ndani yake kulingana na Qira'a ya Abu Ja'far ilikuwa: (لنبوينهم من الجنة غرفا) bila shadda yaani bila idgham. Lakini baadaye aya za Qur'ani ziliwekwa katika kitabu kwa rasm ya Uthmani na kwa haraka (tashkil), hivyo Qira'a ya kwanza ikaja kwa usahihi kulingana na jinsi ilivyothibitishwa katika misahafu ﴿لَنُبَوِّئَـنَّهُم مِّنَ ٱلۡجَنَّةِ غُرَفاً﴾, na wakati mfano ulipotolewa kwa Qira'a nyingine, Qira'a ya Abu Ja'far, inaonekana kuwa mratibu alibadilisha hamza katika matini ya Qira'a ya kwanza na kuweka mahali pake ya kulingana na Qira'a ya Abu Ja'far bila kuzingatia suala la silat mim al-jam' hivyo akaacha haraka kama zilivyokuwa:
(﴿لَنُبَوِّيَـنَّهُم مِّنَ ٱلۡجَنَّةِ غُرَفاً﴾), na hivi ndivyo shadda ilivyoonekana kwenye herufi ya mim katika neno (مّن), na hili ni kosa la uchapishaji...
2- Ama kuhusu maoni yako ya pili kwamba kutoa mfano kwa Qira'a ya Abu Ja'far (لنبوينهم) ni mfano usiofaa kwa sababu (maana ya "بوأ" na "بوا" haitofautiani kwani neno ni lile lile lakini ni kwa hukumu ya ibdal), haya ni maoni yasiyo na usahihi kamili, kwa sababu kutoa mfano katika sehemu hii ya kitabu cha Ash-Shakhsiyyah Al-Islamiyyah ni kwa ajili ya kutumia matamko mawili yanayoashiria maana moja. Hivyo, kutokutofautiana kwa maana hakuathiri usahihi wa mfano, bali kinyume chake, maana inatakiwa iwe moja au inayokaribiana ili mfano uswihi, kwani inasema: (Na hilo limetokea katika Qur'ani kwa kutosheka na baadhi ya maneno badala ya visawe vyake au yanayokaribiana nayo kama vile Qira'at katika Qur'ani), yaani kinachohitajika ni umoja wa maana au kukaribiana kwake pamoja na tofauti ya tamko... Na kutoa mfano kwa Qira'at mbili tofauti kwa sababu ya ibdal ni kutoa mfano kwa matamko mawili tofauti hata kama maana imekuwa moja kabisa, kwa sababu matamko yanayoingiliwa na ibdal ni matamko tofauti na si tamko moja... As-Suyuti aliashiria jambo hili katika kitabu chake (Al-Muzhir) alipozungumzia kuhusu ibdal akasema:
[Aina ya thelathini na mbili: Maarifa ya Ibdal: Ibn Faris amesema katika Fiqh al-Lughah: Miongoni mwa desturi za Waarabu ni kubadilisha herufi, na kuifanya baadhi yake kuwa mahali pa nyingine: madahaha na madahaha, na farasi rifall na rifann, na hili ni jingi na mashuhuri, ambalo wanachuoni wamelitungia vitabu... Na miongoni mwa waliotunga katika aina hii ni Ibn al-Sikkit, na Abu al-Tayyib al-Lughawi.
Abu al-Tayyib amesema katika kitabu chake: Lengo la ibdal si kwamba Waarabu wanakusudia kubadilisha herufi badala ya herufi nyingine, bali hizo ni lugha tofauti kwa maana zinazokubaliana; matamko mawili yanakaribiana katika lugha mbili kwa maana moja, kiasi kwamba hayatofautiani isipokuwa katika herufi moja. Amesema: Na ushahidi wa hilo ni kwamba kabila moja halizungumzi neno wakati mmoja likiwa na hamza na wakati mwingine bila hamza, wala kwa sad mara moja, na kwa sin mara nyingine; na hali kadhalika kubadilisha lam ya utambulisho kuwa mim, na hamza iliyoanzishwa kuwa ayn; kama kauli yao katika mfano wa an kuwa an; Waarabu hawashirikiani katika kitu chochote kati ya hivyo, bali watu hawa husema hivi na wengine husema vile... ] Mwisho.
Hivyo kubadilisha herufi kwa herufi nyingine katika neno moja kunayafanya matamko mawili kuwa tofauti hata kama maana yake ni moja, na hiyo ni kwa sababu kila tamko kati ya hayo mawili ni lugha miongoni mwa lugha za Waarabu: kwani baadhi ya Waarabu husema kuhusu sifa (al-madh) kuwa ni (madah) kwa herufi ha na baadhi yao husema (madah) kwa herufi ha’ na maana ni moja, na baadhi yao husema (saqar) kwa sin na wengine husema (saqar) kwa sad na ndege ni huyo huyo mmoja, na baadhi yao husema (nabu'uhum) kwa hamza na wengine husema (nabuyuhum) kwa ya na maana ni moja... Na Qur'ani Tukufu imetumia katika baadhi ya hali matamko mengi kuelezea maana ile ile katika aya ile ile wakati wa wingi wa Qira'at za Qur'ani za aya hiyo kutokana na wingi wa lugha za Waarabu, na miongoni mwa hayo ni wingi wa lugha kwa sababu ya ibdal kama ilivyo katika sehemu tunayoizungumzia katika kitabu cha Ash-Shakhsiyyah Al-Islamiyyah Juzuu ya Kwanza, kwani tamko la (لنبوئنهم) ni tofauti na tamko la (لنبوينهم) kwa sababu ya ibdal pamoja na kwamba maana ni moja, lakini baadhi ya Waarabu husema (لنبوئنهم) na baadhi yao husema (لنبوينهم), na Qur'ani imetumia lugha hii na ile ambapo Qira'at ziliidadiwa, basi ikawa Qira'a ya baadhi ya wasomaji ni (لنبوئنهم) na ikawa Qira'a ya Abu Ja'far ni (لنبوينهم).
Na kwa hili inadhihirika kuwa hatukukosea tulipotaja Qira'a ya Abu Ja'far (لنبوينهم) kando ya Qira'a (لنبوئنهم) kwa sababu kile kinachohitajika kimefikiwa kwa kutaja Qira'at mbili tofauti ambapo matamko mawili tofauti yanatumiwa kwa sababu ni lugha mbili za Waarabu kuelezea maana ile ile.
Lakini kutoa mfano kwa Qira'a nyingine nayo ni (لنثوينهم) kwa herufi tha mahali pa ba kunaweza kuwa mbali zaidi na kutokea kwa mkanganyiko na kuwa wazi zaidi katika kudhihirisha lile lililokusudiwa katika matini iliyotajwa katika Ash-Shakhsiyyah Al-Islamiyyah na kwa ajili hiyo, tutafanya marekebisho ya matini kwa kuweka (لنثوينهم) kwa herufi tha mahali pa (لنبوينهم) kwa herufi ya.
Hakika Qira'a hii imepokewa kwa aya hiyo hiyo kama ilivyokuja katika An-Nushur fi al-Qira'at al-Ashr: [(وَاخْتَلَفُوا) فِي: لَنُبَوِّئَنَّهُمْ مِنَ الْجَنَّةِ فَقَرَأَ حَمْزَةُ وَالْكِسَائِيُّ وَخَلَفٌ بِالثَّاءِ الْمُثَلَّثَةِ سَاكِنَةً بَعْدَ النُّونِ وَإِبْدَالِ الْهَمْزَةِ يَاءً مِنَ الثَّوَاءِ، وَهُوَ الْإِقَامَةُ، وَقَرَأَ الْبَاقُونَ بِالْبَاءِ الْمُوَحَّدَةِ وَالْهَمْزِ مِنَ (التَّبَوُّءِ) وَهُوَ الْمَنْزِلُ، وَتَقَدَّمَ إِبْدَالُ هَمْزَتِهِ لِأَبِي جَعْفَرٍ فِي الْهَمْزِ الْمُفْرَدِ.] Mwisho. Na ilikuja katika Tafsir al-Tabari: [...{لَنُبَوِّئَنَّهُمْ مِنَ الْجَنَّةِ غُرَفاً} [Al-Ankabut: 58] يَقُولُ: لَنُنْزِلَنَّهُمْ مِنَ الْجَنَّةِ عَلَالِيَ. وَاخْتَلَفَتِ الْقُرَّاءُ فِي قِرَاءَةِ ذَلِكَ، فَقَرَأَتْهُ عَامَّةُ قُرَّاءِ الْمَدِينَةِ وَالْبَصْرَةِ وَبَعْضُ الْكُوفِيِّينَ: {لَنُبَوِّئَنَّهُمْ} [Al-Nahl: 41] بِالْبَاءِ، وَقَرَأَتْهُ عَامَّةُ قُرَّاءِ الْكُوفَةِ بِالثَّاءِ: (لَنُثوِيَنَّهُمْ). وَالصَّوَابُ مِنَ الْقَوْلِ فِي ذَلِكَ عِنْدِي أَنَّهُمَا قِرَاءَتَانِ مَشْهُورَتَانِ فِي قُرَّاءِ الْأَمْصَارِ، قَدْ قَرَأَ بِكُلِّ وَاحِدَةٍ مِنْهُمَا عُلَمَاءٌ مِنَ الْقُرَّاءِ، مُتَقَارِبَتَا الْمَعْنَى، فَبِأَيَّتِهِمَا قَرَأَ الْقَارِئُ فَمُصِيبٌ، وَذَلِكَ أَنَّ قَوْلَهُ: {لَنُبَوِّئَنَّهُمْ} [Al-Nahl: 41] مِنْ بَوَّأْتُهُ مَنْزِلاً: أَيْ أَنْزَلْتُهُ، وَكَذَلِكَ، لَنُثوِيَنَّهُمْ؛ إِنَّمَا هُوَ مِنْ أَثْوَيْتُهُ مَسْكَناً، إِذَا أَنْزَلْتُهُ مَنْزِلاً، مِنَ الثَّوَاءِ، وَهُوَ الْمُقَامُ.] Mwisho.
Na hivyo basi, Qira'at mutawatir kutoka kwa Mtume wa Allah ﷺ kwa ajili ya Qur'ani Tukufu ambazo haiswihi kusoma kwa nyinginezo hazitoki nje ya lugha ya Waarabu:
قُرآنًا عَرَبِيًّا غَيْرَ ذِي عِوَجٍ "Qur'ani kwa Kiarabu isiyo na upotofu." (QS. Az-Zumar [39]: 28)
na hali kadhalika kauli Yake Aliyetukuka:
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ قُرْآنًا عَرَبِيًّا لَّعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ "Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani kwa Kiarabu ili mpate kufahamu." (QS. Yusuf [12]: 2)
yaani kwa lugha ya Waarabu.
Na mwishoni, hakika mimi nathubutisha kwako pupa yako na umuhimu wako katika elimu ya Qira'at na hali kadhalika uchunguzi wako wa usahihi, na namuomba Allah Subhanahu akujalie kheri.
Ndugu yenu Ata bin Khalil Abu Al-Rashtah
23 Rabi' al-Akhar 1443 H Inayoendana na 28/11/2021 M
Link ya jibu kutoka kwenye ukurasa wa Amir (Allah amhifadhi) kwenye Facebook
Link ya jibu kutoka kwenye ukurasa wa Amir (Allah amhifadhi) Web