Home About Articles Ask the Sheikh
Maswali na Majibu

Jibu la Swali: Kusema (as-Salatu Khayrum-minan-nawm) ni Sunnah

March 01, 2019
9708

(Silsila ya Majibu ya Mwanachuoni Mtukufu Ata bin Khalil Abu al-Rashtah, Amir wa Hizb ut-Tahrir, kwa Maswali ya Watumiaji wa Ukurasa Wake wa Facebook "Fiqhi")

Jibu la Swali

Kwa Mohammad AL-khatib

Swali:

Assalam Alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh,

Salamu njema, kisha; nina swali na ninatumai kupata jibu la mkato kwalo.

Je, kusema (as-Salatu khayrum-minan-nawm) katika adhana ya Alfajiri ni uzushi (bid’ah)?

Jibu:

Waalaykum Assalam Warahmatullahi Wabarakatuh,

Swali lako ni kuhusu tathwib, nayo ni: (Muadhini kuongeza msemo wa "as-Salatu khayrum-minan-nawm" mara mbili baada ya maneno ya hay'alatain – yaani hayya 'ala-l-falah – katika adhana ya Alfajiri). Jambo hili si bid’ah, bali ni Sunnah iliyopokelewa kupitia hadithi kutoka kwa Mtume (saw):

1- Abu Dawud ametoa katika Sunan yake kutoka kwa Muhammad bin Abdul-Malik bin Abi Mahdhura, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa babu yake, amesema: Nilisema: Ewe Mtume wa Allah, nifundishe Sunnah ya adhana? Akasema: Basi akapapasa sehemu ya mbele ya kichwa changu, na akasema:

تَقُولُ: اللَّهُ أَكْبَرُ اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ اللَّهُ أَكْبَرُ، تَرْفَعُ بِهَا صَوْتَكَ، ثُمَّ تَقُولُ: أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، أَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ اللَّهِ، أَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ اللَّهِ، تَخْفِضُ بِهَا صَوْتَكَ، ثُمَّ تَرْفَعُ صَوْتَكَ بِالشَّهَادَةِ، أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، أَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ اللَّهِ، أَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ اللَّهِ، حَيَّ عَلَى الصَّلَاةِ، حَيَّ عَلَى الصَّلَاةِ، حَيَّ عَلَى الْفَلَاحِ، حَيَّ عَلَى الْفَلَاحِ، فَإِنْ كَانَ صَلَاةُ الصُّبْحِ قُلْتَ: الصَّلَاةُ خَيْرٌ مِنَ النَّوْمِ، الصَّلَاةُ خَيْرٌ مِنَ النَّوْمِ، اللَّهُ أَكْبَرُ اللَّهُ أَكْبَرُ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ

"Unasema: Allahu Akbar, Allahu Akbar, Allahu Akbar, Allahu Akbar, unanyanyua kwayo sauti yako, kisha unasema: Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, unashusha kwayo sauti yako, kisha unanyanyua sauti yako kwa shahada: Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, Hayya 'ala-s-Salah, Hayya 'ala-s-Salah, Hayya 'ala-l-Falah, Hayya 'ala-l-Falah, na ikiwa ni swala ya Alfajiri, unasema: as-Salatu khayrum-minan-nawm, as-Salatu khayrum-minan-nawm, Allahu Akbar, Allahu Akbar, La ilaha illallah."

Al-Albani amesema hadithi hii ni sahihi. Na Ibn Khuzaymah ametoa mfano wake katika Sahih yake, lakini kupitia njia ya Ibn Jurayj amesema: Aliniambia Uthman bin al-Saib, kutoka kwa mama yake Abdul-Malik bin Abi Mahdhura, kutoka kwa Abi Mahdhura. Kadhalika al-Daraqutni ametoa mfano wake.

2- Katika riwaya nyingine ya Abu Dawud kupitia njia ya Ibn Jurayj, na haya ndiyo matini yake:

حَدَّثَنَا الْحَسَنُ بْنُ عَلِيٍّ حَدَّثَنَا أَبُو عَاصِمٍ وَعَبْدُ الرَّزَّاقِ عَنْ ابْنِ جُرَيْجٍ قَالَ أَخْبَرَنِي عُثْمَانُ بْنُ السَّائِبِ أَخْبَرَنِي أَبِي وَأُمُّ عَبْدِ الْمَلِكِ بْنِ أَبِي مَحْذُورَةَ عَنْ أَبِي مَحْذُورَةَ عَنْ النَّبِيِّ ﷺ نَحْوَ هَذَا الْخَبَرِ وَفِيهِ: «الصَّلَاةُ خَيْرٌ مِنْ النَّوْمِ الصَّلَاةُ خَيْرٌ مِنْ النَّوْمِ فِي الْأُولَى مِنْ الصُّبْحِ...»

Alituhadithia al-Hasan bin Ali, alituhadithia Abu Asim na Abdur-Razzaq kutoka kwa Ibn Jurayj amesema: Aliniambia Uthman bin al-Saib, aliniambia baba yangu na mama yake Abdul-Malik bin Abi Mahdhura kutoka kwa Abi Mahdhura kutoka kwa Mtume (saw) mfano wa habari hii na ndani yake mna: "as-Salatu khayrum-minan-nawm, as-Salatu khayrum-minan-nawm katika (adhana) ya kwanza ya Alfajiri..." yaani si katika ikama, ambayo wakati mwingine huitwa adhana ya pili. Kama ilivyokuja katika hadithi sahihi aliyoitoa al-Bukhari akisema: Alituhadithia Abdullah bin Yazid akasema alituhadithia Kahmas bin al-Hasan kutoka kwa Abdullah bin Buraydah kutoka kwa Abdullah bin Mugaffal amesema: Mtume (saw) amesema:

بَيْنَ كُلِّ أَذَانَيْنِ صَلَاةٌ بَيْنَ كُلِّ أَذَانَيْنِ صَلَاةٌ ثُمَّ قَالَ فِي الثَّالِثَةِ لِمَنْ شَاءَ

"Baina ya kila adhana mbili kuna swala, baina ya kila adhana mbili kuna swala, kisha akasema katika mara ya tatu: Kwa anayetaka."

3- Al-Nasa’i ametoa katika Sunan yake akisema: Alituambia Ibrahim bin al-Hasan akisema alituhadithia Hajjaj kutoka kwa Ibn Jurayj kutoka kwa Uthman bin al-Saib amesema: Aliniambia baba yangu na mama yake Abdul-Malik bin Abi Mahdhura kutoka kwa Abi Mahdhura amesema: Wakati Mtume (saw) alipotoka Hunayn... Mtume (saw) alinikalisha mbele yake akapapasa utosi wangu na kunibariki mara tatu, kisha akasema: Nenda ukaadhini kwenye Nyumba Tukufu (Ka'bah). Nikasema: Vipi ewe Mtume wa Allah? Basi alinifundisha kama mnavyoadhini sasa hivi kwayo:

اللَّهُ أَكْبَرُ اللَّهُ أَكْبَرُ اللَّهُ أَكْبَرُ اللَّهُ أَكْبَرُ أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ أَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اللَّهِ أَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اللَّهِ أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ أَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اللَّهِ أَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اللَّهِ حَيَّ عَلَى الصَّلَاةِ حَيَّ عَلَى الصَّلَاةِ حَيَّ عَلَى الْفَلَاحِ حَيَّ عَلَى الْفَلَاحِ الصَّلَاةُ خَيْرٌ مِنَ النَّوْمِ الصَّلَاةُ خَيْرٌ مِنَ النَّوْمِ فِي الْأُولَى مِنَ الصُّبْحِ...

"Allahu Akbar, Allahu Akbar, Allahu Akbar, Allahu Akbar, Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, (akirejea) Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, Hayya 'ala-s-Salah, Hayya 'ala-s-Salah, Hayya 'ala-l-Falah, Hayya 'ala-l-Falah, as-Salatu khayrum-minan-nawm, as-Salatu khayrum-minan-nawm katika (adhana) ya kwanza ya Alfajiri..."

Al-Albani amesema: Ni sahihi, na kama tulivyotaja awali yaani si katika ikama ambayo pia huitwa adhana ya pili.

4- Al-Bayhaqi ametoa katika Sunan al-Kubra kutokana na hadithi ya Ibn Ajlan, kutoka kwa Nafi’, kutoka kwa Ibn Umar amesema:

كَانَ الْأَذَانُ الْأَوَّلُ بَعْدَ حَيَّ عَلَى الصَّلَاةِ حَيَّ عَلَى الْفَلَاحِ (الصَّلَاةُ خَيْرٌ مِنَ النَّوْمِ) مَرَّتَيْنِ

"Ilikuwa katika adhana ya kwanza baada ya Hayya 'ala-s-Salah, Hayya 'ala-l-Falah (kusemwa) as-Salatu khayrum-minan-nawm mara mbili."

Ibn Hajar amesema: Na sanadi yake ni hasan. Na al-Ya'muri amesema: Na hii ni sanadi sahihi.

Na kama tulivyosema hapo awali, maana ya adhana ya kwanza ni adhana ya Alfajiri na si adhana ya pili yaani ikama, kwani haisemwi katika ikama (as-Salatu khayrum-minan-nawm).

5- Ibn Khuzaymah na al-Daraqutni wamepokea kutoka kwa Anas kwamba amesema: Ni katika Sunnah muadhini anaposema katika Alfajiri Hayya 'ala-l-Falah, aseme as-Salatu khayrum-minan-nawm. Ibn Sayyid al-Nas al-Ya'muri amesema: Nayo ni sanadi sahihi.

6- Ibn Hibban ametoa katika Sahih yake: Alituambia al-Fadhl bin al-Hubab al-Jumahi, amesema: Alituhadithia Musaddad bin Musarhad akasema: Alituhadithia al-Harith bin Ubaid, kutoka kwa Muhammad bin Abdul-Malik bin Abi Mahdhura, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa babu yake, amesema: Nilisema: Ewe Mtume wa Allah (saw), nifundishe Sunnah ya adhana. Akasema: Basi akapapasa mbele ya kichwa changu na akasema:

تَقُولُ: اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ

"Unasema: Allahu Akbar, Allahu Akbar, Allahu Akbar, Allahu Akbar," na akanyanyua kwayo sauti yake, kisha unasema: "Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, na unashusha kwayo sauti yako, kisha unanyanyua sauti yako kwa shahada: Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu alla ilaha illallah, Ash-hadu anna Muhammadan Rasulullah, mara mbili, na Hayya 'ala-s-Salah, Hayya 'ala-s-Salah, Hayya 'ala-l-Falah, Hayya 'ala-l-Falah, na ikiwa ni swala ya Alfajiri unasema: as-Salatu khayrum-minan-nawm, as-Salatu khayrum-minan-nawm, Allahu Akbar, Allahu Akbar, La ilaha illallah."

Hivyo basi, inadhihirika kuwa tathwib katika swala ya Alfajiri ni Sunnah iliyothibiti, na ikiwa kuna maneno yoyote katika baadhi ya riwaya, basi kuna riwaya zilizosahihishwa na baadhi ya watu maarufu wa elimu na kuchukuliwa na mafaqihi wengi. Yaani, tathwib ilikuwepo katika zama za Mtume wa Allah (saw), Makhalifa Waongofu na mpaka leo hii, na si bid’ah bali ni Sunnah iliyothibiti ambayo imekuja na dalili sahihi... kama tulivyobainisha hapo juu.

Natumai jibu hili litakuwa lenye kutosheleza na kukamilika.

Ndugu yenu, Ata bin Khalil Abu al-Rashtah

23 Jumada al-Akhirah 1440 H Mubashara 28/02/2019 M

Kiungo cha jibu kutoka kwenye ukurasa wa Amir (Mungu amuhifadhi) kwenye Facebook

Kiungo cha jibu kutoka kwenye ukurasa wa Amir (Mungu amuhifadhi) kwenye Google Plus

Kiungo cha jibu kutoka kwenye ukurasa wa Amir (Mungu amuhifadhi) Web

Share Article

Share this article with your network