Home About Articles Ask the Sheikh
Maswali na Majibu

Jawabu la Swali: Iran Yakubali Urutubishaji Nje ya Maeneo Yake

May 29, 2010
2269

Swali:

Ni nini kimetokea mpaka Iran ikakubali tena urutubishaji (wa nyuklia) nje ya maeneo yake nchini Uturuki, na kutia saini makubaliano hayo na Brazil na Uturuki?

Jawabu:

Katika kipindi cha hivi karibuni, shinikizo la Ulaya limeongezeka ili kuweka vikwazo vikali dhidi ya Iran kutokana na mpango wake wa nyuklia. Shinikizo hili liliongezeka zaidi baada ya kuingia kwa serikali mpya ya Uingereza, ambayo hata ilitishia hatua za kijeshi. Bila shaka, haiwezi kufanya hivyo peke yake, bali inakusudia kuivuta Marekani katika mivutano na Iran. Aidha, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, William Hague, alielekea Marekani katika ziara yake ya kwanza nje ya nchi baada ya siku tatu tu tangu kuchukua wadhifa wake, ambapo alisisitiza kuwa: "alichagua kwenda Washington katika ziara yake ya kwanza kama waziri wa mambo ya nje wa Uingereza ili kusisitiza uhusiano wa pekee na Marekani" (Asharq Al-Awsat 15/5/2010). Hii ni ishara ya ripoti iliyotolewa na kundi la wanachama wa Baraza la Commons la Uingereza hapo awali, ikitilia shaka uhusiano wa pekee kati ya pande hizo mbili. Kwa hili, William Hague anasisitiza umuhimu wa uhusiano huu na hitaji la Uingereza kwake.

William Hague aliahidi kuishinikiza Iran na alielezea makubaliano yake na msimamo wa Marekani akisema: "serikali yake itafanya kazi ili kuushawishi Umoja wa Ulaya kuchukua maamuzi na hatua kali dhidi ya Iran. Aliongeza: Tumekubaliana juu ya hitaji la kutuma ujumbe mzito na wenye umoja kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, na kupitisha azimio la Baraza la Usalama, na baada ya hapo Uingereza itachukua jukumu muhimu katika kuhakikisha kuwa kuna hatua madhubuti kutoka kwa Umoja wa Ulaya kufuatia azimio kama hilo" (Asharq Al-Awsat 15/5/2010). Ombi lake la kuongeza vikwazo dhidi ya Iran ni kama hatua ya kwanza inayopelekea kupata uhalali wa kimataifa kwa ajili ya hatua za kijeshi. Alisema: "Hatujatofautisha kuunga mkono hatua za kijeshi katika siku zijazo, lakini hatuzilinganii" (Chanzo kile kile). Huu si shinikizo la mazungumzo pekee dhidi ya Iran, bali ni msimamo wa Uingereza. Ilikuwa wazi wakati wa machafuko yaliyoikumba Iran kufuatia uchaguzi wa rais, kwamba Uingereza inajaribu kwa bidii kuuyumbisha utawala wa Iran na kuuangamiza. Inajaribu kutengeneza maoni ya Ulaya yenye shinikizo kwa kushirikiana na Ufaransa na Ujerumani, bila kusahau shinikizo la Israel katika mwelekeo huu. Hivyo, Marekani ilifanya makubaliano na Iran kwa kumteua Rais wa Brazil na Waziri Mkuu wa Uturuki kwenda Iran na kutia saini makubaliano ya kubadilishana urani, na hivyo kusimamisha kasi ya vitisho na vikwazo ambavyo Ulaya ilikuwa ikivipigia upatu, hasa Uingereza na nyuma yake Ufaransa, pamoja na "Israel".

Na hivyo ndivyo ilivyotokea, kwani Iran ilitia saini makubaliano ya mwisho chini ya usimamizi wa Brazil na Uturuki, ambayo yanatamka makubaliano ya Iran kutuma kilo 1200 za urani iliyorutubishwa kwa kiwango cha chini cha 3.5% kwenda Uturuki ili kubadilishwa na kilo 120 za urani iliyorutubishwa kwa kiwango cha juu cha 20%, ambayo inahitajika kwa kinu cha utafiti wa amani kilichopo Tehran. Kiini cha makubaliano haya kilikuwa kimependekezwa na Wakala wa Nishati ya Atomiki (IAEA) ili kutoka katika mkwamo wa mazungumzo kati ya Iran na nchi tano wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama pamoja na Ujerumani takriban mwaka mmoja uliopita, na makubaliano hayo yalifeli wakati huo kutokana na ukosefu wa dhamana na uaminifu.

Vimeongezwa katika makubaliano haya mapya vipengele viwili vikuu vinavyohusiana na dhamana na uaminifu navyo ni:

    1. Urutubishaji uwe nchini Uturuki kama eneo la kati (lisiloegemea upande wowote).
    1. Ikiwa mazungumzo yatafeli kuhusu utekelezaji wa makubaliano haya na kundi la Vienna linaloundwa na Marekani, Ufaransa na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki, basi Uturuki inawajibika kurudisha urani ya Iran iliyorutubishwa kwa kiwango cha chini nchini Iran.

Kwa kuangalia kwa kina makubaliano haya, tunakuta kuwa Marekani ndiyo iliyozihimiza Brazil na Uturuki kusimamia jambo hili. Mtandao wa (France24) ulinukuu: "Marekani, Urusi na Ufaransa zilihikiza rasmi ziara ya 'Lula', Rais wa Brazil, kuelekea Tehran na kuiona kuwa ni fursa ya mwisho ya kuepuka vikwazo." Gazeti la Al-Masry tarehe 18/5/2010 lilichapisha habari hiyo hiyo likinukuu mashirika ya habari ambayo halikuyataja.

Na hadithi ya makubaliano haya ilianza na dhifa ya chakula cha jioni aliyoialika Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Manouchehr Mottaki, kwa wanachama wote kumi na watano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, wakiwemo nchi tano kuu, Uturuki na Brazil ambao ni wanachama wasio wa kudumu katika Baraza la Usalama, pambizoni mwa mkutano wa kufuatilia utekelezaji wa mkataba wa kuzuia uenezaji wa silaha za nyuklia.

Dhifa hiyo ilihudhuriwa na mtu wa pili katika ujumbe wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa, Alejandro Wolff, na walishiriki katika dhifa hiyo wawakilishi katika ngazi ya mabalozi au ngazi za chini kwa wanachama wote kumi na watano wa Baraza la Usalama.

Habari zililimnukuu afisa wa Marekani kabla ya dhifa hiyo akisema: "Marekani inaona dhifa hii kama fursa mpya kwa Iran kuthibitishia Baraza la Usalama kuwa ina uwezo wa kutimiza wajibu wake."

Kufanikiwa kupitishwa kwa makubaliano haya kunamaanisha kuiokoa Iran katika dakika ya mwisho kutoka kwenye vikwazo vya uhakika ambavyo Ulaya ilikuwa ikiviandaa pamoja na Marekani, China, Urusi na Ujerumani, na kuipa Iran angalau miezi mingine mitatu kabla ya kuwekewa vikwazo ikiwa kutatokea tofauti yoyote huko mbele.

Hakuna shaka kuwa hatua ya Uturuki na Brazil ilikuwa kwa maelekezo ya Marekani kwao. Ushahidi ni kwamba Brazil, ambayo ni nguvu ya nane ya kiuchumi duniani, inahitaji Marekani kwa ajili ya kuendelea kukuza uchumi wake, na ilikuwa imetia saini makubaliano ya ulinzi wa kijeshi na Marekani miezi michache iliyopita.

Ama Uturuki, Erdogan, Waziri Mkuu wa Uturuki, alitamka kuwa ataratibu na Marekani moja kwa moja suala la utekelezaji wa vipengele vya makubaliano hayo. Kisha baadaye alitamka kuwa yaliyofanyika yalikuwa kwa uratibu na Washington... na tamko kama hilo lilitolewa na Brazil pia!

Kutegemea kwa Marekani kwa Uturuki na Brazil wakati wa mahitaji kunaisaidia kufanya ujanja katika uwekaji wa vikwazo dhidi ya Iran kama inavyotaka Ulaya na dola ya Kiyahudi kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine kunamaanisha kufaidika kwa Marekani na wanachama wasio wa kudumu katika Baraza la Usalama kwa gharama ya wanachama wa kudumu.

Kwa ufupi, kuingia kwa Uturuki na Brazil kama pande mbili mpya katika faili la nyuklia la Iran kunaisaidia Marekani kuiepusha Iran na pigo lolote au vikwazo vikali vinavyoinyatia, kwa sababu kuingia kwa Brazil na Uturuki katika utiaji saini wa makubaliano hayo ni kuvunjwa kwa wazi kwa umoja wa kile kinachoitwa "jamii ya kimataifa" dhidi ya Iran katika faili hili.

Aidha, makubaliano hayo yameandaliwa kwa lugha ya jumla inayohitaji mazungumzo juu ya utekelezaji wake, na hii inaipa Iran fursa ya kupata pumzi kutokana na shinikizo la jamii ya kimataifa, hasa Ulaya. Iwe makubaliano yatatekelezwa mapema au baadaye, wimbi la shinikizo dhidi ya Iran linatulia hatua kwa hatua, na vivyo hivyo kuiaibisha Marekani kwa upande wa Ulaya na dola ya Kiyahudi ili ichukue hatua ya kijeshi au hata vikwazo vyenye athari halisi; kuiaibisha huku pia kutakuwa kumeondoka.

Share Article

Share this article with your network