Swali:
Imekuja katika kitabu cha Mfumo wa Kijamii (An-Nizham al-Ijtima'i) katika mada ya ndoa ukurasa wa 112 kwenye kitabu kilicho mikononi mwetu, na ukurasa wa 101 kwenye kitabu kilicho katika tovuti rasmi, katika aya ya kwanza inayosema: "Kutokana na mkutano wa wanawake na wanaume huibuka mahusiano yanayohusiana na maslahi yao na maslahi ya jamii wanayoishi ndani yake, nayo ni tofauti na matatizo yanayoibuka kutokana na mkusanyiko katika jamii kwa ajili ya biashara, ukodishaji, uwakilishi na mfano wake. Na inaweza kuja akilini kwamba mahusiano haya ni ndoa pekee...".
Mwanzoni anazungumzia kuhusu mahusiano, kisha anataja kuwa ni tofauti na matatizo, kisha anaendelea kusema "na inaweza kuja akilini kwamba mahusiano haya", kwa nini amesema "nayo ni tofauti na matatizo" na hakusema "nayo ni tofauti na mahusiano" ilhali mazungumzo ni kuhusu mahusiano?
Jibu:
Hakika mfumo katika Uislamu unapanga mambo mawili: Mahusiano, na Matatizo yanayoibuka. Kwa mfano, uhusiano wa mwanamume na mwanamke unapangwa na mfumo wa Uislamu kupitia ndoa. Na yale yanayoibuka kutokana na uhusiano huu miongoni mwa matatizo yanapangwa na mfumo wa Uislamu kupitia talaka kwa mfano. Hivyo, ndoa si mpangilio wa tatizo lililoibuka, bali ni mpangilio wa uhusiano kati ya watu wawili: mwanamume na mwanamke. Na talaka si mpangilio wa uhusiano, bali ni matibabu na mpangilio wa tatizo ambalo linaweza kuibuka kwa kuwepo kwa uhusiano ule... Na uhusiano wa biashara kati ya watu wa jamii unapangwa na Uislamu kupitia mkataba wa mauzo, na yale yanayoibuka kutokana na uhusiano huu miongoni mwa matatizo yanapangwa na mfumo wa Uislamu kupitia hukmu za kuvunja mkataba kwa mfano... Na hivi ndivyo mfumo unavyojumuisha mambo mawili: kupanga uhusiano kwa hukmu za kisheria, na kutibu matatizo yanayoibuka kwa hukmu za kisheria... Katika kitabu cha Mfumo wa Kijamii, kumekuwepo na umakini wa kubainisha mambo haya mawili katika sehemu nyingi za kitabu, yaani umakini wa kuonesha kuwa mfumo wa Uislamu una hukmu zinazopanga mahusiano na hukmu zinazotibu na kupanga matatizo. Hivyo, ni mfumo unaojumuisha nyanja zote. Kwa mfano, imekuja katika kitabu cha Mfumo wa Kijamii yafuatayo:
- Ukurasa wa 6-7 wa kitabu:
(...Zaidi ya hayo, neno (Kijamii) ni sifa ya mfumo, hivyo ni lazima mfumo huu uwe umewekwa kwa ajili ya kupanga matatizo yanayoibuka kutokana na mkutano (ujumuikaji), au kwa ajili ya mahusiano yanayoibuka kutokana na mkutano huo. Na mkutano wa mwanamume na mwanamume, na mwanamke na mwanamke, hauhitaji mfumo kwa sababu hauibuishi matatizo, wala hauibuishi mahusiano yanayohitaji mfumo. Isipokuwa tu kupanga maslahi kati yao kunahitaji mfumo, kwa upande wa kuwa wanaishi katika nchi moja hata kama hawakukutana. Ama mkutano wa mwanamume na mwanamke, na mwanamke na mwanamume, huu ndio ambao huibua matatizo yanayohitaji kupangwa kwa mfumo, na huibua mahusiano yanayohitaji kupangwa kwa mfumo. Hivyo mkutano huu ndio unaostahiki zaidi kuitwa Mfumo wa Kijamii kwa sababu katika uhalisia wake unapanga mkutano kati ya mwanamume na mwanamke, na unapanga mahusiano yanayoibuka kutokana na mkutano huu.) Mwisho.
- Ukurasa wa 100 wa kitabu:
(...Ama yale yanayoibuka kutokana na mkutano huu miongoni mwa mahusiano, na yale yanayotokana nayo miongoni mwa matatizo, hayo ni sehemu nyingine ya mfumo wa kijamii, nayo ni ndoa, talaka, ulezi wa watoto, matumizi (nafaka), na mfano wake. Na hakika, ingawa hukmu hizo - hukmu za ndoa na talaka na mfano wake - ni miongoni mwa mifumo ya jamii, kwa sababu zinapanga uhusiano wa mtu na mtu mwengine, lakini kwa upande wa asili yake zimetokana na mkutano unaofanyika kati ya mwanamke na mwanamume, na kwa ajili hiyo zinajadiliwa kwa upande wa asili yake na chimbuko lake katika mfumo wa kijamii. Ama kwa upande wa maelezo yake ya kina na matawi yake, hizo ni sehemu ya mifumo ya jamii, na zinajadiliwa katika mlango wa miamala.) Mwisho.
Hivyo inabainika kuwa muoano kati ya maneno mawili (uhusiano, matatizo), si maalumu kwa sehemu ile tu iliyoashiriwa na swali katika ukurasa wa 101 wa kitabu cha Mfumo wa Kijamii, na hiyo ni kwa sababu tuliyoitaja ya kutofautisha kati ya uhusiano na tatizo, na kwamba mfumo unajumuisha mambo yote mawili pamoja...
Na kuna jambo lingine nalo ni kwamba sehemu iliyouliziwa inafaa zaidi kutajwa neno "mahusiano" katika nafasi ya kwanza na nafasi ya tatu kwa sababu mazungumzo katika nafasi hizo mbili ni kuhusu jambo lile lile, yaani kuhusu mahusiano ya mwanamume na mwanamke yanayoibuka kutokana na mkutano. Ama nafasi ya pili, ambayo iko katikati, inazungumzia mambo mengine tofauti na mahusiano haya, inazungumzia yale yanayoibuka "kutokana na mkutano katika jamii kwa ajili ya biashara, ukodishaji, uwakilishi na mfano wake". Na biashara, ukodishaji, uwakilishi na mfano wake ni mahusiano kati ya watu, na yale yanayoibuka kutokana nayo inafaa zaidi kutumiwa neno "matatizo" kuliko kutumiwa neno "mahusiano". Na hii hapa ni nakala iliyoashiriwa kwa mara nyingine:
(Kutokana na mkutano wa wanawake na wanaume huibuka mahusiano yanayohusiana na maslahi yao na maslahi ya jamii wanayoishi ndani yake, nayo ni tofauti na matatizo yanayoibuka kutokana na mkutano katika jamii kwa ajili ya biashara, ukodishaji, uwakilishi na mfano wake. Na inaweza kuja akilini kwamba mahusiano haya ni ndoa pekee, na ukweli ni kwamba ndoa ni mojawapo, na kwamba yanajumuisha yasiyokuwa ndoa, na kwa ajili hiyo mkutano wa kijinsia siyo dhihirisho pekee la ghariza ya aina (ghariza an-naw’), bali ni mojawapo ya madhihirisho yake.) Mwisho.
Kwa hili inadhihirika kuwa muoano kati ya maneno mawili (uhusiano, matatizo), ni muoano wa makusudi na una maana yake, na kwamba unaendana pia na muktadha katika sehemu iliyouliziwa, na kwa ajili hiyo haihitajiki kubadilisha maandishi au kuyafanyia marekebisho, kwani ni maandishi yaliyonyooka na yenye mpangilio thabiti.
Natumai kuwa jambo hili limekuwa wazi sasa.
30 Jumada al-Ula 1440 H 05 Februari 2019 M