Home About Articles Ask the Sheikh
Siasa

Barua ya Amir wa Hizb ut-Tahrir, Ata Bin Khalil Abu al-Rashtah, kwa Mutamad wa Wilayah ya Uturuki

July 04, 2005
1611

Amir wa Hizb ut-Tahrir, Ata Bin Khalil Abu al-Rashtah, alituma barua ifuatayo kwa Mutamad wa Wilayah ya Uturuki kufuatia kazi kubwa zilizofanywa na Hizb huko mnamo Ijumaa, 01/07/2005, kwa kusambaza taarifa ya kutetea vazi la stara (khimar) la wanawake watukufu wa Kiislamu nchini Uturuki. Kazi hiyo ilipelekea kukamatwa kwa idadi ya vijana wa Hizb ambao walibaki thabiti kwenye haki, wakipaza sauti zao kwa Takbir na Tahlil bila kuogopa lawama za mwenye kulaumu kwa ajili ya Allah.

Na huu ndio matini ya barua hiyo:

[Ndugu mpendwa Mutamad wa Wilayah ya Uturuki, Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Nimeona yale mliyoyafanya mnamo Ijumaa, 01/07/2005, nayo ni kazi inayoashiria nguvu ya imani vifuani mwa wanaume. Allah awabariki nanyi na kupitia kwenu, Allah awafanyie wepesi ndugu zenu waliokamatwa, na Allah awajaalie ushindi hapa duniani na siku ambayo mashahidi watasimama.

Ndugu mpendwa, Nimeguswa na matukio mawili wakati wa kazi zenu hizi kuu, ambapo matukio hayo yamenirudisha kwenye kipindi cha mwanzo cha Uislamu. Hivyo nilifurahia heri kwamba sisi, akipenda Allah, tunapiga hatua kuelekea kwenye Rayah na Liwa, ambapo kutakuwa na kheri za ardhi na baraka za mbinguni, kwa kusimamishwa kwa Khilafah ya Rashidah ya pili kwa njia ya Utume ambayo ilibashiriwa na Mtume wa mwisho na Imamu wa Mitume.

Ama tukio la kwanza ni la yule mwanamke mwenye subira na anayevumilia huko Van, Mashariki mwa Uturuki, ambapo mwanawe alikamatwa mnamo 17/06/2005 baada ya kutoa taarifa kwa vyombo vya habari mbele ya msititi mkubwa wa Van kuhusu matukio ya Uzbekistan. Alipojua kuwa Hizb itasambaza taarifa ya kutetea vazi la stara (khimar) la wanawake watukufu wa Kiislamu mnamo 01/07/2005, alisema kuwa madhalimu wamemkamata mwanangu wa kwanza, na huyu hapa ni mwanangu wa pili, mchukueni pamoja nanyi katika kampeni yenu ya kutetea vazi la stara la wanawake wa Kiislamu. Mpeni asambaze mnavyotaka, na mtamkuta akiwa imara kwenye haki kama nduguye na kama vijana wenu wote waumini. Kisha akaongeza: "Ni heshima kwetu kuwafikishia watu haki kupitia taarifa zinazobeba maneno ya Allah na kulingania kwenye njia ya Allah," na hakuweza kujizuia akalia sana, na baadhi ya vijana wetu waliokuwepo walilia naye.

Na ama la pili ni kazi kubwa zilizofanywa na vijana wa Bursa wakati wa usambazaji, na haswa ile kauli ya kiuongozi ya Naqib wa mahali hapo alipowahutubia vijana waliopewa jukumu la kuwalinda ndugu zao wakati wa usambazaji kwamba watoe juhudi zao zote kuwalinda ndugu zao dhidi ya udhia wa madhalimu hata kama wao wenyewe watapatwa na udhia huo. Hakika ni dhabihu inayokumbusha Salaf (watangulizi) wema walio tutangulia kwa imani.

Sijui kama huyu Naqib uliyemtaja kwa jina la (Serdar) ni yule tunayemjua au ni mwingine. Vyovyote vile, Allah amlipe kheri. Na barua hii ni kwake yeye, kwa chombo cha mahali hapo, na kwa vijana wa Bursa:

(Ndugu mpendwa Naqib wa mahali hapo, Bursa Ndugu wapendwa wanachama wa mahali hapo, Bursa Ndugu wapendwa vijana wa mahali hapo, Bursa

Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Zimetufikia habari za ushujaa wenu katika kusambaza taarifa ya khimar ya wanawake watukufu wa Kiislamu, na kukabiliana kwenu na madhalimu kwa neno la haki bila kuogopa lawama za mwenye kulaumu kwa ajili ya Allah, na bila kudhoofishwa na mikusanyiko yao na uvamizi wao wa kinyama dhidi yenu. Na ikiwa mashujaa ishirini na tano kati yenu wamekamatwa kutokana na hilo, basi huo ni mzunguko katika njia ya Allah. Watatoka humo, akipenda Allah, wakiwa na afya tele na nguvu zaidi, wakifagia udhalimu na giza, na kupasua njia kuelekea kwenye nuru katikati ya umati, huku mbele yao kukiwa na sauti za Allahu Akbar na wakifunikwa na kivuli cha bendera ya Uislamu.

Enyi Ndugu:

Mmeandika kurasa zilizojaa kheri kwa wino safi na mnyofu. Na lile tendo lenu la kuwaokoa akina dada wawili watukufu kutoka mikononi mwa madhalimu ni kielelezo kikubwa kitakachotajwa kwenu katika mizani ya mema yenu, akipenda Allah.

Nawatumia salamu, na namuomba Allah kwa ajili ya waliokamatwa wapate faraja ya haraka, msamaha, afya njema, na malipo ya dhati. Na kwenu nyote msaada kutoka kwa Allah (swt), kinga dhidi ya kila baya, na hifadhi dhidi ya kila shari.

Wassalamu Alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh. 03/07/2005 Ndugu yenu) mwisho wa barua.

Wassalamu Alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh.

27 Jumada al-Ula 1426 H 04/07/2005 M

Amir wa Hizb ut-Tahrir Ata Bin Khalil Abu al-Rashtah

Share Article

Share this article with your network