Ni upi hukumu ya kuuza pesa kwa pesa?
Maadamu mada ya mauzo ni pesa kwa pesa, basi inaingia chini ya hukumu za sarfu. Ili sarfu iwe sahihi, lazima iwe:
a) Papo hapo (hadhiran bi hadhirin): Katika hali hii, ikiwa ni jinsi (aina) moja, lazima iwe mkono kwa mkono na kwa usawa (kiasi kile kile). Ikiwa ni jinsi mbili tofauti, basi ni mkono kwa mkono upendavyo. Dalili za hilo zinajulikana, miongoni mwazo ni: Mtume wa Allah (saw) amesema:
الذَّهَبُ بِالذَّهَبِ وَالْفِضَّةُ بِالْفِضَّةِ وَالْبُرُّ بِالْبُرِّ وَالشَّعِيرُ بِالشَّعِيرِ وَالتَّمْرُ بِالتَّمْرِ وَالْمِلْحُ بِالْمِلْحِ مِثْلًا بِمِثْلٍ سَوَاءً بِسَوَاءٍ يَدًا بِيَدٍ فَإِذَا اخْتَلَفَتْ هَذِهِ الأَصْنَافُ فَبِيعُوا كَيْفَ شِئْتُمْ إِذَا كَانَ يَدًا بِيَدٍ
"Dhahabu kwa dhahabu, fedha kwa fedha, ngano kwa ngano, shayiri kwa shayiri, tende kwa tende, na chumvi kwa chumvi; mfano kwa mfano, sawa kwa sawa, mkono kwa mkono. Na vikihitalifiana aina hizi, basi uzianu upendavyo ikiwa ni mkono kwa mkono." (Imepokelewa na Muslim kupitia Ubada bin al-Samit)
b) Ainisho na dhima (aynan wa dhimmatan): Inajuzu kulipa thamani ya mauzo kwa pesa ile ile "mada ya thamani" au kwa bei ya siku hiyo kutoka kwa pesa nyingine mkono kwa mkono. Dalili yake ni hadith ya Ibn Umar (... basi ninauza kwa dinari na kuchukua dirham, na ninauza kwa dirham na kuchukua dinari, nikichukua hizi badala ya hizi, na kutoa hizi badala ya hizi. Mtume wa Allah (saw) akasema:
لا بأس أن تأخذها بسعر يومها ما لَم تفترقا وبينكما شيء
"Hakuna neno kuichukua kwa bei ya siku hiyo maadamu hamujaachana na huku hakuna kitu kilichobaki kati yenu (deni)." (Hadith ya Ibn Umar)
Hii inaashiria kujuzu kwa kubadilisha thamani thabiti katika dhima (deni). Hii ni sarfu ya ainisho (ayn) na dhima. Lakini ni lazima makabidhiano yawe mkono kwa mkono.
c) Sarfu katika dhima (sarfan fid-dhimmah): Kwamba mtu awe na deni la dhahabu katika dhima ya mwingine, na huyo mwingine awe na deni la fedha katika dhima ya mtu wa kwanza, kisha wakabadilishana kile kilicho katika dhima zao, kwa kulipa kile kilicho katika dhima yake cha dhahabu kwa kile alicho nacho cha deni la fedha. Jambo hili linajuzu kwa sababu dhima iliyopo ni sawa na ainisho iliyopo, mradi tu mada hiyo imalizike katika kikao kile kile. Suala hili linaitwa katika fiqh (As-Sarfu fid-Dhimmah).
25 Dhul-Hijjah 1424 H 16/02/2004 M